
Hatimaye Mungu amejibu maombi ya wakristo wengi waliochukua muda kumuombea mchungaji Saeed Abedini baada ya kuachiwa huru toka gerezani nchini Iran ambako aliwekwa kizuizini kwa kosa la kuhubiri injili nchini humo miaka takribani minne iliyopita. Mchungaji Saeed ambaye ni raia wa Marekani lakini mzaliwa wa Iran aliachiwa huru siku ya jumamosi iliyoisha, baada ya kuwepo shinikizo kubwa kutoka kwa serikali ya Marekani, taasisi za haki za binadamu bila...